Monday, October 29, 2007

KWA HERI SHUJAA LUCKY DUBE!


NITAMKUMBUKA LUCKY DUBE SIKU ZOTE ZA MAISHA YANGU!





KWA HERI SHUJAA LUCKY PHILIP DUBE



Natafuta namna ya kuanza kuandika makala hii, kwa sababu nataka iwe makala maalumu kabisa, na zaidi sana nataka iwe tuzo kwa kazi ya nzuri ya Lucky Philip Dube wakati wa uhai wake duniani. Mbali na serikali ya Afrika ya kusini kumzawadia kombe la dunia la Rugby ambalo nchi hiyo ilitwaa baada ya kuifunga Uingereza, nataka makala hii iwe pia zawadi ya rambirambi kwa familia ya mwanamuziki huyo na Afrika kwa ujumla.

Unaweza ukauliza pengine, kwamba kama makala hii inamhusu Lucky Dube kwa nini basi isiwe kwenye kurasa za michezo na burudani? Sikiliza ndugu yangu, kwa upande wangu mwenzako Lucky Dube hakuwa mwanamuziki na mleta burudani, kwangu dube alikuwa ni mwanaharakati kama wanaharakati wengine duniani. Ndio maana inawashangaza watu kuona Mwinjilisti kama mimi kuanza kuzungmzia habari za Lucky Dube, na uzuri sikumficha mtu, nilisema wazi nimefiwa, nimeumizwa na kifo cha ndugu huyu wa Afrika.

Nilishaacha kusikiliza nyimbo za Lucky dube, na badala yake mpaka mauti ina mkuta nilikuwa nikizisoma na kuzitafakari, zilikuwa kama hotuba za kiongozi Fulani kwangu, nilimchukulia sawa na kina Nelson Mandela na kina Martin Luthere King, Jr.

Kuna mambo mengi yanayonifanya nimtofautishe Dube na wanamuziki wengine na hasa wale wa rege, kwa mfano matumizi ya bangi, pombe na imani kwamba haile Selassie alikuwa au ni Mungu, haya na mengine yalinifanya nimheshimu Dube na kumtenga na baadhi ya wanamuziki wenzake wakiwemo wa Tanzania. Nimewahi kubishana sana na wenzangu kuhusu imani ya Dube, hasa nilipokuwa shule ya msingi pale Gilman Rutihinda pale Dar es salaam, wengi waliamini kwamba, eti kwa sababu tu alikuwa na rasta kichwani, basi yeye ni ‘rastafarian’ na pia kwamba kwa sababu aliimba rege, pengine ni kutokujua kwamba rege ni aiana ya mahadhi Fulani ya muziki na kwamba hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya rege na bangi, mimi niliamini kuwa Dube ni mkristo kwa dini, nah ii ilitokana na baadhi ya maneno ya baadhi ya nyimbo zake, kigezo kingine ni kwamba nyimbo nyingi za Lucky Dube zimeakisi ukweli kuhusu maisha yake mwenyewe aliyoyapitia.

Fuatilia nyimbo kama slave, remember me, think about the children na it’s not easy, katika mabishano hayo jamaa zangu waliendelea kushikilia misimamo yao ile, lakini Lucky Dube mwenyewe alipokuja Dar mwaka 1997 aliwahi kusema hivi “kama urastafarian ni kufuga rasta, kuvuta bangi na kunywa pombe na kuamini Haile Selassie ni Mungu basi mimi si Rastafarian, lakini kama ni itakuwa ni kuhusu siasa na maisha ya kila siku basi mimi ni Rastafarian”

Kwangu tofauti kubwa iliyoko kati ya Lucky Dube na wanaharakati na wanafalsafa wengine kama Mwalimu Nyerere wa Tanzania, Nelson Mandela, Martin Luther na wengine ni kwamba wao walikuwa hawaimbi lakini wote walitumia majukwaa kueneza ujumbe kwa hadhira yao na malengo yao yalifanana, wote ni wapambanaji, kama huamini sikiliza kauli aliyoitoa Dube mwaka 2000, hapa anasem,a hivi “A lots of people were thinking that once we had this black government everything would be fine, may be we were only fighting the past government because it was a white government. But that is not the case with me, I was just fighting the system, it is the same now, if there is injustice or any sort of nonsense towards people I will sing about that” akiwa na maana kwamba, watu wengi walifikiri kwamba baada ya kuwa na serikali ya watu weusi kila kitu kinge kuwa sawa, pengine tulikuwa tukipambana na tu na serikali ya zamani kwa sababu tu ilikuwa ni serikali ya weupe (Makaburu) lakini sivyo ilivyo kwangu, nilikuwa napambana na mfumo, na ndivyo ilivyo sasa, kama kuna namna yoyote ya uonevu na upuuzi wowote wanaofanyiwa watu (raia) nitaimba hilo nalo”

Hii si kauli ya mtu wa kawaida, ni kauli inayoweza kutolewa na wanaharakati jasiri tu kama Lucky Dube, na ukiwa makini utagundua kupitia kauli yake kwamba hakuwa mpigania haki wa Afrika tu bali pia wa Ulimwengu. Anasema ili mradi serikali hiyo inafanya ndivyo sivyo dhidi ya wananchi wake yeye ataimba. Na kupitia Dube ndipo pia unaweza kuona umuhimu wa kuwa na wagombea binafsi wa kizalendo, wao mara nyingi hawana muda wa kusiamam na kutetea maslahi ya vyama vyao au serikali za dhalimu, maana hata kama wangetaka kusiama upande wa wananchi katiba au kanuni za vyama vyao zingewabana. Hujawahi kusikia wanasiasa wanaolalamikia au kukosoa mwenendo mbaya wa vyama dhidi raia wao wanaambiwa apaleke hoja zake kwenye vikao? Wanafanya hivyo huku wakielewa fika kwamba wataminywa na kunyamazishwa. Sijaelewa hasa kwa upande wa Tanzania kwa nini bado kuna ugumu kuruhusu wagombea binafsi kama walivyo dai watu kama Faustine Munishi na Christopher Mtikila, wanahofu kitu gain?

Lucky Dube aliimba na kusema ukweli bila kuogopa Taifa, chama au serikali Fulani. Fuatilia wimbo kama Puppet masters, No truth in the World, Victims, na You stand alone utalewa nini nasema hapa.
Fuatilia wimbo wake wa 'Crazy World hapa uone
So far so good we still living today
But we don't know what tomorrow brings
In this crazy world
People dying like flies every day
You read about it in the news
But you don't believe it
You'll only know about it
When the man in the long black coat
Knocks on your door'Cause you're his next victim
As you are living in this
Chorus:Living in, living in this crazy world (x4)
Leaders starting wars every time they want
Some for their rights,
Some for fun and their own glory
letting people die for the wrong that they do
Oh it's painful
come on now little boy
Say your prayers before you sleep
Little boy went down on his knees
And he said:"Oh Lord Now I lay me down to sleep
I pray the Lord my soul to keep
And if I die before I wake
I pray the Lord my soul to take.
"'Cause he's living in this crazy worldOh Lord
Mpaka hapa sasa angalau tunaishi, lakini hatujui kesho italeta nini,
Katika ulimwengu huu uliochanganyikiwa,
Kila siku Watu wanakufa kama inzi,
Unayasoama haya kwenye taarifa za habari lakini huamini,
Unakuja kujua mpaka pale mtu mwenye koti jeusi anapokujia
Na kugonga mlangoni kwako, Kwa sababu wewe ndiwe mhanga wake
Unapoishi kwenye ulimwengu huu ulio changanyikiwa
Viongozi huanzisha vita kila wakati wanapojisikia,
wengine wa kutetea haki zao na wengine kwa ajili ya mambo ya ajabu na kujitafutia tu utkufu
Wanaaacha watu wanakufa kwa amakosa wanayofanya wao, Ooh inaumiza
Ee mvulana mdogo, fanya sala kabla hujalala, Yule kijana akapiga magoti na kusema,
Ee Bwana Sasa nalala, Namuomba Bwana roho yangu ailinde, Na kama nitakufa kabla sijaamka
Namumba Bwana roho yangu aichukue, Kwa sababu anaishi kwenye ulimwengu huu uliochanganyikiwa!

Lucky Dube aliwashinda hata baadhi ya wanasiasa kwa moyo wa upendo kwa watu wake, na kwa moyo huo ndio maana mmoja wa mawaziri nchi Rwanda katika salamu zake za rambirambi amesema wamempoteza rafiki yao . Ni nadra sana kwa viongozi wa kitaifa kutoa kauli zao kwenye vifo vya wana muziki wengie wa kawaida, ndio maana nakwambia kwa watu wanaofuatialia masuala ya kiutawala, haki na usawa watakubaliana na mimi kuwa Dube hakuwa tu mwanamuziki bali mwanaharakati hasa, hilo linaweza lisisemwe wazi au hadharani na wanasiasa lakini wanaelewa mishale yake, nah ii ni hasa kwa wanasiasa wakorofu, waonevu na wadhalimu dhidi ya wananchi wan chi zao. Dube alikuwa makini kwa maana ya kuijua historia ya Afrika na jamii yake.

Alitembelea Rwanda mara tu baada ya mauaji ya halaiki mwaka 1994, mauaji ambayo hayatasahaulika kwa vizazi hivi vya karibuni, huko alifanya maonesho kwenye jiji la Kigali kwenye uwanja wa mpira wa Amahoro (Amani) na moja kati ya nyimbo zilizowatoa Wanyarwanda machozi ni ule wa ‘together as one’ sehemu ya wimbo huo inasema hivi


In my whole life,My whole life I've got a dream (x2)

Too many peopleHate apartheid Why do you like it? (x2)

Chorus: (x3)Hey you rasta manHey European,Indian man, We've got to come together as one

Not forgetting the Japanese


The cats and the dogsHave forgiven each otherWhat is wrong with us (x2)All those yearsFighting each otherBut no solution (x2)


Kwa kiswahili anasema. Katika Maisha yangu yote nimekuwa na ndoto, watu wengi hawapendi ubaguzi wa rangi, kwa nini wewe unapenda, enyi marastafariani, wazungu na wahindi tunatakiwa kuwa kitu kimoja

Paka na mbwa walisameheana, tatizo ni nini kwetu? Miaka yote hii tumepigana wenyewe kwa wenyewe bila suluhisho,


unaonaje wewe ujumbe huu, je haukuwa mahususi kwa Wanyarwanda kwa wakati ule? Bila shaka aliimba pia ule wimbo wake wa “we cray for peace’ (tunalilia Amani)
Katika wimbo huo anasema “tunalilia Amani kamili, Ee Mungu tunalilia upendo katika ujrani huu, nakwambia hakuna maji yanayoweza kuzima moto huu (vita) Ni Mungu peke yake anaweza kutuokoa”
Kuanzia wiki ijayo nitakuletea maelezo na tafsiri ya baadhi ya nyimbo zake kwa wiki mbili ikiwa ni ishara ya watoto wawili wa Dube walioshuhudia mauja ya baba yao.

Dube pia atakumbukwa na watu masikini duniani kwa sababu ya kuwatetea, aliwashukia matajiri wa ulimwengu kwa kusema utajiri wao hakuwa na maana yoyote duniani kama watakuwa hawawajali masikini na wale watu wasio na matumaini katika wimbo wake wa ‘hand that giveth’
Sasa LUCKY PHILIP DUBE hayupo tena, wamekatisha uhai wake kwa risasi, mtu ambaye pamoja na kwamba hakunifahamu nilimuombea ampe Yesu maisha yake, niliwahi panga siku moja kwamba siku za usoni ningemtembelea Afrika ya kusini ili kumshirikisha neno la Mungu, sasa katoweka na ndoto zangu zimezimika. Naanza kurudi nyuma kukumbuka jinsi alivyonifanya nitoroke shule kwenda kumpokea uwanja wa ndege Dar es salaam na alipokuwa anaorudi kwao nilitega shule kuhakikisha kuwa naenda kumuaga, nakumbuka nilipokuwa nagombana na mama nyumbani kwa sababu ya kupiga kanda zake mfululizo na kuziimba pia kwa sauti, nakumbuka nilipogombana na walimu kama vile mwalimu Sadala na mwalimu Assey pale Rutihinda kwa kutembe kila wakati huku nikiimba nyimbo za Dube, nilipotumia nyimbo zake kama mifano katika mazungumzo na rafiki zangu na katika baadhi ya makala zangu, Bila shaka wakina Simba Ramadhani, George Madanga, Hafidh Ismail, Juma, Humphrey Mutabirwa na Ukasha Mrami wanakumbuka nilivyokuwa kituka kwa kuwehuka na mwanaharakati huyo, ndio maana pamoja na kuelewa kwamba hivi sasa mimi ni mchungaji bado hawajaacha kunitumia salamu za pole! Hayupo tena! Tuonane wiki ijayo kuendelea na maombolezo na kumbukumbu hii muhimu katika maisha yangu!