Thursday, May 24, 2007

NDESANJO MACHA TUSAIDIE!

Ndesanjo unisamehe buree, nimeitumia picha yako hapa! Naona uko na mheshimiwa Michuzi!


Salaam kwa wanablogu za kiswahili wowote na popote mlipo!
Pengine salaam hizi ni maalum zaidi kwa Ndesanjo Macha kule USA! Huyu ndiye aliyenichochoea na kunielimisha kupitia makala zake katika gazeti la Mwananchi jumapili. Naam, nilitoka jasho kwelikweli, nilidhani ni kazi kweli kufungua blogu, mpaka nikafikia hatua ya kumuomba Ndesanjo anifungulie mwenyewe!


Hatimaye! Nasema hatimaye nimefungua blogu yangu sasa, uwanja wa kusemea yale yaliyo mawazo yangu, sasa ombi langu ni kwako Ndesanjo, naomba unisaidie namna ambavyo nitajiunga na ule umoja wa wana blogu za kiswahili! Kila la heri na YESU ANAKUPENDA!