Friday, June 8, 2007

USIOGOPE!


Ni mchana huu wa leo, tunajiandaa na mitihani ya kumaliza mwaka na wakati huo huo kampeni za kuwania urais hapa chuoni kwetu zimeanza, kwa hiyo pia tumetoka kuwasikiliza wagombea, hawana tofauti sana na wanasiasa wa vyama vya siasa. Maneno meeengi. Tunasubiri utekelezaji, ndipo tutakapoweza kuhukumu ikiwa walitaka umaarufu au kututumikia wanafunzi!
Ni hatari sana kama wanataka kujifunzia siasa hapa chuoni, ni sawa ikiwa tui watakuwa hawajifunzi kudanganya kama walivyowaongo wanasiasa wengi Tanzania (na duniani?? au?)
Nyota njema huonekana asubuhi, msemo huu haujachuja maana yake bado, bado unafanya kazi. Chuoni ni mahali pa kujifunza uadili na ubadhirifu ukitaka. Kinachonisikitisha ni kwamba hata wasomi nao huwa bado hawana macho ya kung'amua waongo wanaodanganya mchana kweupee! Hivi mtu na akili zako unachagua kiongozi chuoni eti kwa sababu kakuahidi atahakikisha tunapata mikopo bila kutueleza njia atakazozitumia.
Atatupatiaje na kwa njia zipi? Mashaka zaidi tunayapata kwa sababu mtoa ahadi hizo hachukui mkpo, analipiwa na wazazi aua anajilipia mwenyewe. Huo ni mtihani mdogo sana wa wasomi kuwapima wanaotaka uongozi. Ndio maana wale wale wanaisasa wakija na sera zao kuwa watatujaza mapesa tunashangilia kana kwamba ana ghala za pesa sehemu fulani. oooh! samahani, naomba niishie hapa kwa leo! Nawahi kujiandaa na mitihani!


Nazungumzia hapa Chuo Kikuu cha Tumaini-Dar es salaam. Huyu anaitwa Anisa Juma, baada ya kujisomea, sasa ni mapumziko ikiwa ni pamoja na kupiga picha.