Wednesday, May 23, 2007

Na sisi tunazo jamani!





Kuna watu wanafikiri mimi Mkenya kwa kuifagilia Windsor, jamani penye ukweli si tunapaswa kusimama? Hizo hapo juu ni baadhi ya Hoteli zetu nzuri hapa Zipo zingine kule Zanzibar. Kwa leo nimekutafutia hizi.
Ya kwanza kule juu ni Movenpick Hotel, iko mtaa wa Ohio jijini Dar es salaam, imeshabadilishwa majina mara kibao, inadaiwa kuwa wanakwepa kodi, mabepari (wawekezaji) ndio wamiliki tofauti na ile ya Kenya. Ingine ni Kilimanjaro Kempisk, zamani iliitwa Kilamnjaro Hotel, nashukuru tu, katika kukarabati kwao (maana hukarabati mpaka majina) jina la mlima wetu limebaki. Kwa mujibu wa mtandao Hoteli zote hizi mbili zina hadhi ya nyota tano! 5* star