Monday, June 11, 2007

SINZA INATIA AIBU KWA UCHAFU!

Huu ni moja tu kati ya mitaa michafu ya kule kunakoitwa Sinza kwa wajanja! Huu ni mtaa maarufu wa Sinza Msikitini au, wakazi wanapita kwenda maofisini, sidhani hata kama kuna mtu mmoja anawaza cha kufanya!


Huwezi amini kuwa hii ni Sinza, hawa ni watoto niliwafunmania asubuhi na mapema wakicheza kwenye uchafu uliolundikwa njiani na watu wenye akili timamu, si hivyo tu, lakini wanachezea pia maji machafu. Watu wanaodhaniwa kuwa ni wazazi wao walikuwepo nikipiga picha!

WAKAZI WA SINZA WANASEMA WAO SI DAWASCO WALA SERIKALI, NI KAMA VILE WANA 'ENJOY' SANA KUISHI NA UCHAFU


Huu ni mtaa anaoishi Mwenyekiti wa Serikali za mitaa Sinza, nyumba iliyojaa nyasi hapo kushoto ni nyumba ya kidosi mmoja, na kulia ni nyumba ya kidosi mwingine, wanatoka na magari yao na kuacha midimbwi hiyo kila siku kana kwamba hawaoni, Ili mradi wana masofa ya kutoka Ulaya ndani na vitu vingine vya thamani yakiwemo magari haoni haja ya kuweka mtaa safi!
Niliwahi kumfuata Mwenyekiti na kumuuliza kulikoni, akasema yeye hana la kufanya, eti hana la kufanya kiongozi, mbona kama ni viongozi Tanzania tumepata!