Friday, May 25, 2007
Ni kama vile nasema "ole wenu ninyi waandishi, mnaonunuliwa na wakubwa na kuikosesha jamii ya watanzania haki ya kuhabarishwa! hakuna, kataeni, muwe na huruma na jamii ambayo inawategemea kuwasemea kule ambako wao hawawezi kusema!
Ni haki yetu kusema, kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania 18(a)
Thursday, May 24, 2007
NDESANJO MACHA TUSAIDIE!
Salaam kwa wanablogu za kiswahili wowote na popote mlipo!
Pengine salaam hizi ni maalum zaidi kwa Ndesanjo Macha kule USA! Huyu ndiye aliyenichochoea na kunielimisha kupitia makala zake katika gazeti la Mwananchi jumapili. Naam, nilitoka jasho kwelikweli, nilidhani ni kazi kweli kufungua blogu, mpaka nikafikia hatua ya kumuomba Ndesanjo anifungulie mwenyewe!
Hatimaye! Nasema hatimaye nimefungua blogu yangu sasa, uwanja wa kusemea yale yaliyo mawazo yangu, sasa ombi langu ni kwako Ndesanjo, naomba unisaidie namna ambavyo nitajiunga na ule umoja wa wana blogu za kiswahili! Kila la heri na YESU ANAKUPENDA!
Wednesday, May 23, 2007
Na sisi tunazo jamani!

Kuna watu wanafikiri mimi Mkenya kwa kuifagilia Windsor, jamani penye ukweli si tunapaswa kusimama? Hizo hapo juu ni baadhi ya Hoteli zetu nzuri hapa Zipo zingine kule Zanzibar. Kwa leo nimekutafutia hizi.
Ya kwanza kule juu ni Movenpick Hotel, iko mtaa wa Ohio jijini Dar es salaam, imeshabadilishwa majina mara kibao, inadaiwa kuwa wanakwepa kodi, mabepari (wawekezaji) ndio wamiliki tofauti na ile ya Kenya. Ingine ni Kilimanjaro Kempisk, zamani iliitwa Kilamnjaro Hotel, nashukuru tu, katika kukarabati kwao (maana hukarabati mpaka majina) jina la mlima wetu limebaki. Kwa mujibu wa mtandao Hoteli zote hizi mbili zina hadhi ya nyota tano! 5* star
Tuesday, May 22, 2007
WINDSOR GOLF HOTEL & COUNTRY HOTEL
Watu kama sisi tulilala vyumba kama hivi, nafikiria kufanyia 'Honey Moon' yangu hapa!
Jengo hili la kwanza ndio kila kitu, mapokezi, sehemu ya chakula na vinginevyo, lakini yale majengo yanayofuatia ni vyumba vya kulala wageni
Hii ndio Windsor unavyoweza kuina kwa juu, nyuma kuleeee, ni jiji la Nairobi
Hii ni Hotel ambayo tulifikia tukiwa jijini Nairobi, sio siri nili 'enjoy' kwelikweli, siku moja nitakupa stor kuhusu Hoeli hii. lakini moja ya mambo yaliyonifurahisha ni kwamba, ni Hoteli kubwa ya kimataifa, yenye hadhi ya nyota tano 5* Hotel inayomilikiwa na Mkenya tena ameajiri wazungu katika Hoteli hiyo.
Monday, May 21, 2007
Nyerere analia au anacheka?
Najaribu kuwaza ikiwa watu wangekuwa wanakufana na kisha kupewa nafasi ya kurudi duniani, naamini pengine Nyerere angelia, si kuja duniani tu, hata ingekuwa kwamba wafu wangekuwa wanaruhisiwa kupokea taarifa mbalimbali kutoka duniani, tabasamu hili la hayati Nyerere lisingeonekana! Angekuwa analia! sababu unazijua!
MATUMIZI YA PESA ZA UMMA!
Ni muhimu mara nyingine kukaa pamoja na kujadili masuala mbambali yanayohusu taifa letu. Hii ni moja ya mijadala ya wanafunzi kuhusu matumizi ya pesa za wananchi. hapo niliigiza kama waziri wa habari, utamaduni na michezo. Chuo kikuu cha Tumaini Iringa. Kushoto ni Jozaka na yule binti pale anaitwa Caroline na yule mwenye upara ni Balikudembe
Wednesday, May 16, 2007
UZINZI HAUGOPI SIASA WALA DINI YAKO!
Huyu anaitwa mheshimiwa Amina Chifupa, mmoja wa vyanzo vya habari vya makala hii! Hapa alikuwa akila kiapo cha kuwa muadilifu (bungeni)
Nimechukua hatua kuandika makala hii kufuatia matukio mawili yaliyotokea hivi karibuni. Tukio la kwanza ni la Mbunge wa viti maalumu wa UVCC Amina Chifupa wa Mpakanjia, mitaani amepewa majina mengi sana, mengine siwezi hata kuthubutu kuandika hapa. Huyu ametengana na mumewe Mohamed Mpakanjia au Med.
Tukio la pili ni lile la Padri mmoja huko Arusha kutuhumiwa kuhusika na utoaji mamba, halafu walio andika wanasema eti katoa mimba katika mazingira yasiyo safi na salama, kwa maneno mengine mauji ya kiumbe aliyekuwa tumboni yamefanyika katika mazingira yasiyo safi na salama, kwa hiyo kuna dalili kwamba kama mauaji hayo yasingefanyika katika mazingira hayo basi yangekuwa halali.
Hilo sio hoja yetu ya leo, suala ni kwamba Padri Staphene Uhuru alikuwa anashiriki ngono na mwanafunzi wa kidato cha pili wilayani Mbulu, huyu dada sasa ni marehemu. Padri kakiuka maadili ya kikatoliki yanayomtaka kwamba sio kufanya ngono tu bali hata kuoa. Wengi wameshangazwa na tukio hili, tukio hili lina mlolongo. Kwanza jamaa kutembea na kibinti cha kidato cha pili, pili kutoa mimba, tatu mauaji.
Mimi sikushangazwa na lolote kati ya hayo, kwa sababu yako, ni ya kawaida. Waulize wanafunzi watakuambia. Kuna madai kuwa walimu nao hufundisha kwa nadharia na vitendo masomo ya kibaiolojia. Yaani uhusiano wa mwalimu na mwanafunzi haushii katika taaluma tu, bali mpaka kwenye mahaba. Taarifa hizi zipo! Ni unafiki kukataa! Kwa hiyo sio la ajabu mwanafunzi kufanya mapenzi, maana ni kama tabia mashuleni. Kutoa mimba nalo sio la ajabu, tembelea shule za bweni, naambiwa mimba hutolewa mabwenini.
Tujadili kitendo cha Padri kushiriki ngono, wengi niliwasikia wakijadili kama vile ni tukio la ajabu. Walichokuwa wanashangaa sio ngono, walikuwa wanashangaa kwamba Padri kafanya ngono.
Ili mada yetu inoge, turudi kidogo kwa Amina Chifupa, kilichomtenga na mumewe? Amina anadaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Zito Kabwe mbunge wa CHADEMA, Zito mwenyewe amekanusha tuhuma hizo. Vyovyote iwavyo, kilichomfanya Amina apewe talaka ni uhusiano wake usiofaa na Mheshimiwa Kabwe tena huku akiwa na ndoa yake. Tusirefushe mambo, kwenye ndoa ni rahisi kusema amina kaachwa kwa tuhuma za uzinzi, Kwa hiyo Amina anatuhumiwa kwa uzinzi!kwani uhusiano usiofaa wanaouzungumzia ni upi?
Kwamba watu wanashangaa matukio kama ya Amina na yule Padri ni ukweli kwamba binadamu huwa tunasahau kuwa watu kama wanasiasa na viongozi wa dini ni binadamu kama tulivyo, hilo huwa tunalisahau! Kama mchungaji mmoja kule Korogwe alivyo wahi kusema kwamba zamani alikuwa anaamini kuwa Wazungu huwa hawaendi haja kubwa, alisahau kuwa nao ni binadamu kama sisi Wanyakyusa na Wangoni.
Tukio la pili ni lile la Padri mmoja huko Arusha kutuhumiwa kuhusika na utoaji mamba, halafu walio andika wanasema eti katoa mimba katika mazingira yasiyo safi na salama, kwa maneno mengine mauji ya kiumbe aliyekuwa tumboni yamefanyika katika mazingira yasiyo safi na salama, kwa hiyo kuna dalili kwamba kama mauaji hayo yasingefanyika katika mazingira hayo basi yangekuwa halali.
Hilo sio hoja yetu ya leo, suala ni kwamba Padri Staphene Uhuru alikuwa anashiriki ngono na mwanafunzi wa kidato cha pili wilayani Mbulu, huyu dada sasa ni marehemu. Padri kakiuka maadili ya kikatoliki yanayomtaka kwamba sio kufanya ngono tu bali hata kuoa. Wengi wameshangazwa na tukio hili, tukio hili lina mlolongo. Kwanza jamaa kutembea na kibinti cha kidato cha pili, pili kutoa mimba, tatu mauaji.
Mimi sikushangazwa na lolote kati ya hayo, kwa sababu yako, ni ya kawaida. Waulize wanafunzi watakuambia. Kuna madai kuwa walimu nao hufundisha kwa nadharia na vitendo masomo ya kibaiolojia. Yaani uhusiano wa mwalimu na mwanafunzi haushii katika taaluma tu, bali mpaka kwenye mahaba. Taarifa hizi zipo! Ni unafiki kukataa! Kwa hiyo sio la ajabu mwanafunzi kufanya mapenzi, maana ni kama tabia mashuleni. Kutoa mimba nalo sio la ajabu, tembelea shule za bweni, naambiwa mimba hutolewa mabwenini.
Tujadili kitendo cha Padri kushiriki ngono, wengi niliwasikia wakijadili kama vile ni tukio la ajabu. Walichokuwa wanashangaa sio ngono, walikuwa wanashangaa kwamba Padri kafanya ngono.
Ili mada yetu inoge, turudi kidogo kwa Amina Chifupa, kilichomtenga na mumewe? Amina anadaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Zito Kabwe mbunge wa CHADEMA, Zito mwenyewe amekanusha tuhuma hizo. Vyovyote iwavyo, kilichomfanya Amina apewe talaka ni uhusiano wake usiofaa na Mheshimiwa Kabwe tena huku akiwa na ndoa yake. Tusirefushe mambo, kwenye ndoa ni rahisi kusema amina kaachwa kwa tuhuma za uzinzi, Kwa hiyo Amina anatuhumiwa kwa uzinzi!kwani uhusiano usiofaa wanaouzungumzia ni upi?
Kwamba watu wanashangaa matukio kama ya Amina na yule Padri ni ukweli kwamba binadamu huwa tunasahau kuwa watu kama wanasiasa na viongozi wa dini ni binadamu kama tulivyo, hilo huwa tunalisahau! Kama mchungaji mmoja kule Korogwe alivyo wahi kusema kwamba zamani alikuwa anaamini kuwa Wazungu huwa hawaendi haja kubwa, alisahau kuwa nao ni binadamu kama sisi Wanyakyusa na Wangoni.
Ndivyo ilivyo, tunawachukulia wanasiasa na watu wa dini kama vimiungu kama sio miungu. Eti tunashangaa Padri kuzini, cha ajabu kipi wakati yeye naye ni mwanaume lijali? Tunachoshangaa ni nini kusikia Amina kaachika kwa tuhuma za uzinzi? Mbona Amina kaanza kutuhumiwa toka akiwa Makongo Sekondari, tangu akiwa mtangazaji wa Clouds FM?
Napenda nikukumbushe kwamba suala la ngono (sio mapenzi, mapenzi ni ya wanandoa) haliko kama wengi wanavyodhani, kama ni mchzo, basi ngono ni wa aina yake! Ngono(uzinzi) si tabia kama unavyoweza kufikiri! Ni muhimu kuelewa kwamba mtu mzinzi ni mzinzi hataka kabla hajalala na mwanaume au mwanamke ambaye si mkewe/mumewe. Kama alivyo mwizi, hawi mwizi baada ya kuiba, huwa mwizi hata kabla hajaiba na muongo vivyo vivyo! Ndio maana naamini kwamba mzinzi hafugiki hataka kama ni mkeo au mumeo, uzinzi ni ugonjwa, ni kichaa cha kiwango cha juu sana.
Asipozini kwa kulala na mwanaume/mwanamke, basi atazini katika akili au moyo wake, ndio maana Yesu alitangaza
“Mmesikia kwamba imenenwa Usizini. Lakini mimi nawaambia, kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, amkwisha kuzininaye moyoni mwake”
Mathayo 5:27-28 Upo mpaka hapoo?? Kuzini ni kitendo kinachoanzia moyoni, moyo ambao kila mwanasiasa anao, kila shehe na kila mchungaji anao.
Ninachotaka kusema hapa ni kwamba, uzinzi ni roho au roho chafu (evil spirits) inayotenda kazi ndani ya mtu. Roho ninayoizungumzia hapa si ule uhai wa mtu. Kwa imani yangu mimi (Mkristo) kuna kiumbe kinaitwa Ibilisi, yeye huwa na idara katika utendaji wake. Kwa maneno mengine, zile idara ni mawakala wa Ibilisi duniani. Kazi ya mawakala hawa ni kuhakikisha kwamba mwanadamu anakwenda kinyume na kila kilichoagizwa na Mungu. Mawakala hawa pia huitwa pepo wachafu (demons) hutmia nguvu za kishetani (demonic power) kufanya kazi ndani ya mtu bila kujali hadhi au cheo chake ndani ya jamii. Ndio maana sio ajabu Stephen Uhuru kuzini japo ni Padri ambaye akiwa madhabahuni husimamisha mishipa kuwataka watu waache uzinzi. Sio ajabu kumkuta Shehe akifanya zinaa na mke wa jirani yake japo hukauka koo akiwataka watu kuacha maovu, na sio ajabu tena kumkuta mwanasiasa bila haya usoni akituma dereva wake kwenda shule moja wapo ya sekondari ili akamtafutie binti wa kuvinjari nae! Sio ajabu, maana kuna roho inatenda kazi ndani yake.
Nimekwambia Ibilisi ana mawakala, hawa hufanya kazi tofauti tofauti, kuna wale wanohakikisha binadamu anakuwa mdhulumaji au wezi, ndio maana sio ajabu kukuta wanasiasa wezi, wanaowaibia wananchi wao, ni roho! Kuna mawakala wa ibilisi wanaohakikisha kuwa watu wanakuwa wanafiki, wafitini, wagomvi na wazinzi! Mawakala hawa ni kuhakikisha kuwa mwanadamu anakwenda kinyume na kila jema aliloagiza Muumbaji wa Mbingu na nchi.
Ndio maana kwenye Warumi 8:6-7 inasema
“Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani. Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kutii”
Mwanadamu ana roho na mwili, mwili una nia ya mauti, na ndio maana tunauzika ardhini, na tunaamini pia kuwa roho inapaa na kwenda kwa Mungu aliyeiumba.
Soma na hapa tena Wagalatia 5:17
“Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka”
Bila shaka unaanza kupata picha ya kile ninachotaka ujue. Kwamba mara nyingine watu hufanya uzinzi si kwa sababu wanapenda, ni kama kitu Fulani huwapekesha ndani. Na mujibu wa Biblia, Mungu alijua kuwa hii miili ina matatizo yake, hata hivyo hakuhalalisha dhambi kwa kigezo kwamba miili ina matatizo, bali amesema
“Kila mmoja wenu (nikiwemo mimi) ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima, si katika hali ya tama mbaya kama mataifa wasiomjua Mungu” 1Wathesalonike 4:4-5
“Basi nasema enendeni kwa roho, wala hamtazitimiza kamwe tama za mwili” Galatia 5:16
Wengine hufikiri kwamba watu hufikia hatua ya kufanya uzinzi ili kujipatia kipato, hii ina maana kwamba wale wenye kiapato kizuri hawafanyi uzinzi. Hapana! Ukitaka kuamini, mchukue binti yako, mpe kila kitu nyumbani kwako, mpe gari ya kutembelea, mwekee viyoyozi kuanzia sebuleni, chumbani, stoo, jikoni mpaka chooni! Chukua pesa ndio ziwe zuria la nyumba nzima, au mpe pesa ziwe mataulo ya kujifutia baada ya kuoga.
Mpe pesa zingine ziwe vitambaa vya kushonea nguo zake za kuvaa, au ziwe leso za kuvutia jasho baada ya mazoezi ya viungo. Kwa kufupisha, muulize mahita ambayo anadhani akipata ataridhika kuwapo duniani, kasha mpatie, mi nakwambia kama na ile roho, hatachukua hata siku mbili, kwanza ataona pesa ulizo mpa ni utumwa!
Hii ni kukuonesha kwamba, uzinzi si tabia kama tabia zingine, ni roho inayofanya kazi kuupelekesha mwili, ndio maana nikasema, mtu huweza kuwa mzinzi hata kama hakutaka kuwa hivyo!
Tukirudi kwa upande wa Amina na yule padri sasa utaanza kuelewa kwa nini nilikuambia uzinzi haujali hadhi ya mtu katika jamii yake. Yalimpata Bill Clinton wa Marekani, mtu aliyeheshimika dunia nzima. Kama utakuwa unafahamu siri hutashngaa kwamba kwa nini na wao hufanya uzinzi.
Kuna watu walifikiri kuwa kuoa ni suluhisho, kwamba wataacha tabia hii chafu watakapopata waume au wake zao. Ndugu zangu waislamu, sheria zao zinaruhusu kuoa mke zaidi ya mmoja, lakini wataniunga mkono nikisema kwamba bado kuna wanaotoka nje ya ndoa, wapo wanaobadili wanawake kama mashati. Wanawake nao hawako nyumba katika mchezo huo, bila haya mtu huweza kuchukua mume wa mtu na kuishi naye, na mwanaume kuacha mke na kutembea na mwanamke mwingine. Hili lipo katika jamii, watu wanafikiri ni tabia ya kawaida kama ilivyo tabia ya watanzania kuwakarimu wageni au wachaga kupenda mtori!
Ni idara maalumu ya Ibilisi inayotenda kazi ndani ya watu, ni kampeni ya Ibilisi kwa kila mtu ili tuache kuyafanya ya mwenyezi Mungu. Hata hivyo hatuwezi kuendelea kuwa wazinzi kwa kisingizio kwamba sio sisi bali ni Ibilisi. Wakati wa kushiriki tendo hilo hakuna ambaye anakuwa hajui kuwa anafanya nini, kila mtu anajua, au kama ni mawazo ni wazi kwamba kila mtu anakuwa anajua anawaza nini. Kumbuka tulivyosoma hapo juu, haya ni mashindano ya mwili na roho, ni vita kali roho inasema sitaki, mwili unasema nataka, Biblia imetuapa jibu kwamba tusienende kwa mwili bali kwa roho, tena tumeambiwa kwamba kila mtu ajue kuuweza mwili wake!
Nina ujasiri wa kutumia Biblia hapa kwa sababu huwa naamini kuwa Biblia sio ya wakristo peke yao, ni ya waislamu pia, ndio maana hutumika kuwazodoa Wakristo kwenye mihadhara ya Kiislamu, na mara nyingine nimesikia ikisomwa misikitini! Si sahihi kwa Wakristo kusema Biblia ni mali yao! Tunapaswa kushinda!
Hebu soma kipengele hiki ambacho Mungu alikuwa akizungumza na mtoto wa mwanadamu wa kwanza, yaani Adam, mtoto huyu aliitwa Kaini.
“Kama ukitenda vyema, je hutapata kibali? Usipo tenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde” Mwanzo 4:7
Unaona hapo? Kumbe dhambi ipo, inaweza kumuotea mtu (kummendea, kumvizia ili imshinde) pia dhambi inaweza kumtamani mtu kwa lengo la kumfanya ashindwe kufanya yaliyo ya MUNGU, kama inaweza kutamani maana yake ina tambuzi wa namna Fulani, ndio maana nikakwambia, dhambi ni roho inayotenda kazi. Pamoja na hayo, bado Kain anaambiwa inampasa kuishinda. Kwa nini? Alikuwa anajua anachofanya tangu alipokuwa anawaza.
Kaini alikuwa anapanga kumuua ndugu yake aliyeitwa Habili, tayari Mungu aliliona hilo, akamtahadharisha Kaini juu ya kile alichotaka kukifanya, kwamba kilikuwa ndani yake ndio, kiliingia pengine bila Kaini kupenda, hilo halina ubishi, lakini alipaswa kushinda! Tukijaaliwa siku moja tutaangalia namna tunavyoweza kuushinda uzinzi!
0713 550 778
ilovejesustz@yahoo.com
Subscribe to:
Posts (Atom)






